• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAKURUGENZI KASIMAMIENI USAFI KWENYE MAENEO YENU – RC MHITA

Posted on: September 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita ametoa agizo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri mkoani humo kuhakikisha wanasimamia kikamilifu hali ya usafi wa mazingira kuanzia ngazi ya Kitongoji/Mtaa, Kijiji hadi Kata, kama sehemu ya utekelezaji wa ajenda ya Afya ya Jamii na Mazingira Salama.

Akizungumza leo Septemba 16, 2025, wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mikataba ya Lishe kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Mhita amesema kuwa suala la usafi ni ajenda ya kudumu inayohitaji uwajibikaji wa pamoja na ufuatiliaji wa karibu kutoka kwa viongozi wa ngazi zote.

“Kila Jumamosi iwe ni siku ya usafi wa mazingira katika maeneo yote ya Halmashauri, na Jumamosi ya mwisho wa mwezi ifanyike usafi mkubwa unaojumuisha mitaro, masoko, maeneo ya wazi na taasisi.” amesisitiza Mhe. Mhita.

Mkuu wa Mkoa pia ametumia nafasi hiyo kusisitiza umuhimu wa utekelezaji wa Mkataba wa Lishe, akiwataka watendaji kuhakikisha Siku za Afya na Lishe za Vijiji zinafanyika ipasavyo, zenye lengo la kutoa elimu ya lishe, kupima hali za watoto na kutoa rufaa za haraka kwa wanaohitaji msaada wa kiafya.

Vilevile, alielekeza kuwa kila shule ya msingi na sekondari kuhakikisha watoto wanapata chakula cha mchana shuleni, jambo ambalo linachochea afya bora, ufanisi wa ujifunzaji na mahudhurio ya wanafunzi.

“Shule zisizo na mpango wa chakula ni lazima zianzishe haraka, hili ni suala la kipaumbele. Hatutaki kuona mtoto anasoma akiwa na njaa, ni jukumu letu kuhakikisha hilo linatimia,” alisisitiza.

Mhe. Mhita alihitimisha kwa kusema kuwa maendeleo ya sekta ya afya na elimu hayawezi kutenganishwa na usafi wa mazingira na lishe bora. Hivyo, viongozi wote wanapaswa kuona kuwa ni wajibu wao kuhimiza, kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa maelekezo hayo kwa vitendo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa