• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAMILIKI WA VITUO VYA KULELEA WATOTO MCHANA SHINYANGA WAASWA KUSAJILI VITUO VYAO ILI KUTOA HUDUMA SALAMA KWA WATOTO

Posted on: August 20th, 2025

Wamiliki wa Vituo vya Kulelea Watoto Mchana (Day Care Centres) katika Manispaa ya Shinyanga wamehamasishwa kuvisajili vituo vyao kwa mujibu wa sheria na taratibu ili kuhakikisha watoto wanaolelewa katika vituo hivyo wanakuwa katika mazingira salama, rafiki na yanayozingatia haki za mtoto.

Wito huo umetolewa na Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Bi. Sarah Sanga, wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha wamiliki wa vituo hivyo, kilichofanyika jijini Shinyanga.

Bi. Sanga amesisitiza kuwa ni muhimu kwa kila mmiliki kuhakikisha kituo chake kimesajiliwa rasmi na kina cheti halali kilichosainiwa na Kamishna wa Ustawi wa Jamii, kama uthibitisho wa kutambuliwa na Serikali.

“Ninawasihi na kuwahamasisha wamiliki wote wa vituo vya kulelea watoto mchana kuvisajili vituo vyao ili vitambuliwe rasmi. Lengo letu ni kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama na yenye staha. Usajili huu ni kinga kwa watoto, kwa wamiliki na kwa jamii,” alisema Bi. Sanga.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Shinyanga, Bi. Lydia Kwesigabo, alisema kuwa kikao hicho ni sehemu ya maandalizi ya Wiki ya Ustawi wa Jamii inayotarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 25 hadi 30, 2025, ambapo pamoja na elimu, huduma za usajili wa vituo zitatolewa.

Aliongeza kuwa usajili huo utasaidia kuimarisha huduma zinazotolewa na vituo hivyo, pamoja na kujenga mtandao rasmi wa umoja wa wamiliki wa vituo katika mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kubadilishana uzoefu na uboreshaji wa huduma.

Akizungumza kwa niaba ya wamiliki wa vituo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Vituo vya Kulelea Watoto Mchana, Bi. Damari Morris, aliwahimiza wamiliki wote ambao hawajasajili vituo vyao kutumia fursa ya Wiki ya Ustawi wa Jamii kujitokeza kwa ajili ya kusajili na kurasimisha huduma zao.

Kwa ujumla, kikao hicho kilitambua mchango wa vituo vya kulelea watoto mchana katika ukuaji wa mtoto, huku kikisisitiza umuhimu wa kufuata miongozo ya serikali ili kuwalinda watoto dhidi ya mazingira hatarishi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO KAZI CHA MMMAM CHAFANYIKA SHINYANGA, KUWEKA MIKAKATI MADHUBUTI YA MALEZI NA MAKUZI BORA KWA MTOTO

    August 20, 2025
  • WAMILIKI WA VITUO VYA KULELEA WATOTO MCHANA SHINYANGA WAASWA KUSAJILI VITUO VYAO ILI KUTOA HUDUMA SALAMA KWA WATOTO

    August 20, 2025
  • RC MBONI MHITA ATETA NA MANAIBU WAZIRI KUHUSU AJALI YA MGODI WA NYANDOLWA – ATANGAZA MAENDELEO YA ZOEZI LA UOKOAJI

    August 19, 2025
  • RC MBONI MHITA APONGEZA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA KWA KUIMARISHA MAADILI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI.

    August 19, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa