• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wanafunzi wahimizwa kutumia vizuri michezo ya UMISSETA kupata ajira

Posted on: May 28th, 2017

Mashindano ya michezo kwa shule za sekondari (UMISSETA) Mkoani Shinyanga, yamefunguliwa rasmi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya kitaifa ya UMISSETA yatakayofanyika Mkoani Mwanza.

Akifungua mashindano hayo yaliyofanyika katika shule ya sekondari Don Bosco Didia Wilayani Shinyanga, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewataka wanafunzi kutumia vizuri viwanja vya michezo kuonesha vipaji na uwezo wao ili ipatikane timu itakayowakilisha vizuri kitaifa.

Mkuu wa Mkoa amewaeleza wanamichezo hao kuwa michezo ni ajira, afya na furaha hivyo wasiache hata kwa ambao hawatapata nafasi ya kuwakilisha kitaifa. Telack amewaambia kuwa wakijituma watapata ajira kupitia michezo itakayowapeleka kitaifa na kimataifa akitolea mfano wachezaji wanaoiwakilisha Tanzania katika michezo mbalimbali kimataifa.

Mhe. Telack amesema, Serikali itahakikisha wanafunzi hao wanaofikia 598 na walimu 54 wanakaa vizuri kambini hapo ili wafanye vizuri katika maandalizi hayo.

Telack pia ameishukuru kampuni ya vinywaji baridi ya Coca Cola kwa kudhamini mashindano hayo, ambapo amepokea vifaa mbalimbali vya michezo ikiwemo jezi na mipira itakayopelekwa kwenye shule zote za Sekondari Mkoani hapa.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Mkoa Bw. Albert Msovela amemshukuru Mhe. Telack kwa kuyapa uzito na umuhimu mkubwa mashindano hayo ambapo timu ya Mkoa itakayopatikana itaenda kushindana Kitaifa. 

Msovela amesema anaamini vijana hayo wameandaliwa na watajiandaa vizuri na wana ari kubwa hivyo ni hazina kubwa ya Taifa ambayo baadaye itakuwa ni wawakilishi wazuri hata Kimataifa.

Amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa, itakuwa ni fursa nzuri kwa wanafunzi hawa baada ya mashindano wataweza kushiriki na kuutangaza Mkoa katika nyanja mbalimbali kupitia ushiriki na ushindani wao. Hivyo walimu wahakikishe wanapata timu nzuri itakayowakilisha vema.

Aidha, Msovela ametumia nafasi hiyo kuzipongeza timu mbili za Stand United na Mwadui kwa kufanya vizuri katika mashindano ya ligi kuu ya Tanzania hivyo kuutangaza Mkoa wa Shinyanga katika tasnia ya Michezo, hivyo anaamini vijana hao wanafunzi watatengeneza pia nafasi kwa siku za baadaye baada ya kumaliza masomo yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUOMBA NAFASI YA UJUMBE WA BODI YA HOSPITALI YA MKOA January 03, 2020
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha nne 2019 January 09, 2020
  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa Kidato cha pili 2019 January 09, 2020
  • Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Shinyanga May 07, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU 100

    June 27, 2021
  • SIKU MIA 100 ZA RAIS SAMIA

    June 27, 2021
  • DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

    June 05, 2021
  • Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga aapishwa

    June 02, 2021
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa