• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wananchi watakiwa kukaa mbali na maeneo ya Kambi za Jeshi kuepuka madhara

Posted on: December 4th, 2019

Wananchi wametakiwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi kulinda mipaka ya Kambi na kukaa mbali ili kujiepusha na madhara yanayoweza kutokea kwa sababu ya mazoezi mbalimbali ya Jeshi yenye lengo la kulinda usalama wa Raia.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack ameyasema hayo jana tarehe 03/12/2019 katika Mkutano na wananchi wa Kijiji cha Mwamashele, Kata ya Kizumbi, Manispaa ya Shinyanga ambapo wananchi hao walidai wamezuiliwa kufanya shughuli za kilimo kwenye eneo la Jeshi.

Mhe. Telack amesema  ni agizo la Serikali maeneo yote ya Jeshi nchi nzima kuwekwa mipaka hivyo wananchi hao waendelee kulima maeneo mengine waliache eneo la Jeshi ili wasije kupata madhara iwapo yatatokea kutokana mazoezi ya Jeshi.

Amesema ana taarifa zote kuwa wananchi walikuwa wanalima eneo hilo la Kizumbi na kama Serikali inafurahishwa na jambo hilo kwa sababu wanazalisha lakini kwa usalama wao na Taifa kwa ujumla ni vema kukaa mbali kwani kutoka na changamoto za Kiusalama zinavyoongezeka na miundombinu ya usalama inaongezeka pia ikiwemo maeneo.

"Kambi zote zitawekwa mipaka kwa usalama wa wananchi, maeneo ya kulima yapo tusiingie eneo lililozuiliwa mtapata madhara hivyo tushirikiane kwa pamoja kama wananchi kulinda kambi yetu na tusiokote kitu chochote tusichokijua ili kujiepusha na matatizo" amesisitiza Mhe. Telack.

Mkuu wa Idara ya Ardhi katika Manispaa ya Shinyanga Bw. Kenneth Chande ametumia nafasi hiyo pia kuwafafanulia wananchi hao sheria ya ardhi kuhusu fidia ambapo walidai wananchi wengine walilipwa lakini wenyewe hawakulipwa na kuwaeleza kuwa, wananchi waliolipwa kipindi hicho ardhi inatwaliwa na Jeshi, walilipwa fidia ya eneo lililokuwa limeendelezwa wakati huo.

Naye Kiongozi wa Jeshini hapo amesema eneo hili lilitengwa kwa ajili ya mafunzo ya Jeshi hivyo amewaomba wananchi kuacha kufanya shughuli ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa