• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wananchi watakiwa kutopeleka Serikalini mashauri yaliyopo Mahakamani

Posted on: February 6th, 2020

Wananchi wametakiwa kuacha kupeleka kwenye Ofisi za Wakuu wa Wilaya na Mikoa malalamiko yanayolenga mashauri ambayo tayari yapo mahakamani.

Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya Sheria leo tarehe 06/02/2020, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewaeleza wananchi kuwa, Serikali haifanyii kazi mashauri hayo kwa sababu tayari yanashughulikiwa na mahakama ambayo ndiyo yenye majukumu ya kupokea na kutatua mashauri.

Mhe. Telack amesema kuwa, Serikali inashirikiana kwa karibu na mahakama kuhakikisha haki inatendeka kwa wananchi wote. "Nikiwa nafahamu kuhusu shauri ambalo lipo mahakamani nitawasiliana na Jaji na kumpa dondoo kuhusu shauri hilo ili aweze kupata mwanga na kufanya maamuzi kwa usahihi"

Akifafanua suala la baadhi ya watu kulalamikia watu kuwekwa ndani na Wakuu wa Mikoa na Wilaya, Telack ametoa wito kwa wananchi kuwa, hakuna mwananchi aliye juu ya sheria hivyo, mtu yeyote anayevunjwa sheria atawajibishwa. Telack amefafanua kuwa, nafasi za Wakuu wa Wilaya na Mikoa ni za Serikali hivyo wanasimamia shughuli zote ndani ya maeneo yao husika na iwapo wananchi wakiona mtu kawekwa ndani basi kuna jambo amefanya.

"Kuna mahali lazima Serikali itumie nguvu, ukisikia mtu kawekwa ndani na Mkuu wa Wilaya au Mkoa ujue lipo jambo amelifanya, kama kuna dalili za uvunjifu wa amani lazima hatua zichukuliwe, mengine tusipoyafanya hata nyie wananchi yanawaathiri" amesisitiza Telack.

Awali akitoa neno kwa niaba ya Chama cha Wanasheria Kanda ya Shinyanga Bw. Mbatina ameshauri Serikali iongeze rasilimali watu kwenye Mahakama ili kutatua tatizo la mashauri kuchukua muda mrefu kumalizika. 

Mbatina amesema kuwa, Mahakama ina wajibu wa kuhakikisha mashauri yanayopelekwa yanamalizika kwa wakati na kwa haraka.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiingia katika eneo la maadhimisho ya siku ya Sheria Mkoa wa Shinyanga, Mahakama Kuu kanda ya Shinyanga akiwa ni mgeni mahususi

Mawakili, Wanasheria na Mahakimu wakiwa wamejipanga tayari kwa maandamano kuadhimisha siku ya Sheria



Maandamano yakiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu kanda ya Shinyanga Mhe. Gerson Mdemu kuelekea eneo la maadhimisho


Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga Mhe. Gerson Mdemu, akikagua gwaride maalumu kwa ajili ya siku ya Sheria katika viwanja vya Mahakama Kuu Mjini Shinyanga

Shekh Soud Kategile, kwa niaba ya Shekh Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga akiomba dua kabla ya kuanza shughuli za maadhimisho ya siku ya Sheria

Askofu Emmanuel Makala wa Kanisa la KKKT akiomba kabla ya kuanza shughuli za maadhimisho ya siku ya sheria


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akicheza pamoja na wanakwaya wa Kanisa la AICT Kambarage Shinyanga wakati wakitumbuiza siku ya Sheria Mkoani hapa

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Sheria kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akicheza pamoja na kikundi cha Shinyanga Artist wakati wakitumbuiza siku ya Sheria

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa