• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

Posted on: September 27th, 2025

Watendaji wa Vyama Vikuu vya Ushirika (AMCOS) kutoka Mkoa wa Tabora wametakiwa kufanya kazi kwa ubunifu, maarifa na uadilifu ili kuongeza uzalishaji na thamani ya mazao ya biashara kama tumbaku, pamba na mazao mchanganyiko kwa manufaa ya wakulima na uchumi wa mikoa yao.

Wito huo umetolewa Septemba 26, 2025 na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi – Utawala na Rasilimali Watu, Bw. David Lyamongi, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya vitendo kwa watendaji wa AMCOS, yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Kampasi ya Shinyanga.

Lyamongi amesema mafunzo hayo ni nafasi ya kipekee kwa watendaji hao kujifunza namna bora ya kusimamia ushirika na kuwa chachu ya mabadiliko katika uzalishaji wa mazao ya biashara nchini.

“Mnapaswa kuwa wabunifu, msiwe wa kawaida. Ushirika wenu ndio dhamana ya wakulima, hivyo mnapaswa kuwapa maarifa, teknolojia na mbinu za kuongeza thamani ya mazao yao. Tutumie mafunzo haya kujijenga na kuleta matokeo chanya mashinani,” amesema Lyamongi.

Aidha, aliwataka viongozi hao kuendesha vyama vyao kwa uadilifu na ufanisi, wakizingatia Sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 6 ya mwaka 2013, huku wakiepuka ubadhirifu, uzembe na matumizi mabaya ya madaraka ili kudumisha imani ya wanachama na kuongeza mafanikio ya vyama vyao.

Kwa upande wake, Kaimu Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Tabora Jarufu Juma, amesema mafunzo hayo ya siku 14 yamelenga kuwajengea uwezo watendaji ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kuleta matokeo chanya kwenye vyama vyao.

“Watendaji wetu wako tayari kujifunza na kutumia mafunzo haya kama chachu ya mabadiliko. Tunataka AMCOS zetu ziwe sehemu ya suluhisho la kiuchumi, si changamoto kwa wakulima,” amesema Jarufu.

Mafunzo hayo yanayoshirikisha zaidi ya washiriki 120, yanatarajiwa kuwa kichocheo cha mageuzi katika usimamizi wa AMCOS na kuinua uchumi wa wakulima kupitia ushirika imara, unaozingatia tija, ubunifu na uwajibikaji.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa