• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WA SACCOS YA MGODI WA MWADUI YAFUFULIWA NA KUKABIDHIWA LESENI YAO YA SACCOS NA CHETI

Posted on: July 5th, 2023

Na, Shinyanga RS.

Mrajis MSaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga leo tarehe 5 amekabidhi Leseni ya daraja “B” kwa Mwadui SACCOS na Cheti cha usajili kwenye mkutano wa wanachama wa Mwadui SACCOS. Ambao umehudhuriwa pia na Mmiliki wa Mgodi ambae pia ni mwajiri wa watumishi hawa Bw. Isack Mtoni Gamba.

Pamoja na kuwakabidhi Leseni yao ya biashara na cheti lakini pia amewapongeza Bodi iliyopo kwa kushirikiana na wanachama wake kwa kuonesha ushirikiano mkubwa wakati wa ufufuaji wa chama hiki.

Chama hiki cha akiba na mikopo cha watumishi wa Mwadui SACCOS kilianza mgogoro tangia Mwaka 2013 baada ya uongozi wa chama kufuja pesa za wanachama wake na kupelekea chama kushindwa kutoa mikopo na hata mikopo kwa wanachama wake. Mwaka 2017 baada ya uliokua uongozi wa bodi kutosimamia chama hiki kwa uamini na uadilifu na kupelekea fedha za wanachama kupotea.

Ofisi ya Mrajis kwa kushirikiana na Afisa ushirika na Uongozi wa bodi imeanza harakati za kusaidia kufufua SACCOS hii tangia mwaka2021 kwa kuondoa uongozi uliokifikisha chama kwenye hasara hii baada ya kufanyika kwa uchunguzi na kubaini madeni hayo.

Tume ya maendeleo ya ushirika Nchini katika kuhakikisha madeni haya yanarejeshwa imemleta mkusanya madeni ambae hivi sasa ameanza kazi rasmi na atashirikiana na uongozi mpya ili kusaidia madeni hayo kurejeshwa ili kuongeza mtaji wa chama. Ofisi imeendelea kuhamasisha wanachama wake kuona namna bora ya kuweza kukusanya madeni hayo na kuwashawishi kushirikiana kufufua SACCOS yao.

“Lakini pia tunamshukuru mwajiri wao kampuni ya Williumson ya Mwadui kukiwezesha chama hiki na kuonesha nia ya kukisaidia ili kiweze kusimama Kwakua watumishi hao wa mgodi walionesha umuhimu wa kuwa na SACCOS katika eneo la kazi itakayowasaidia kukidhi mahitaji yao ya kifedha na kwa riba nafuu kwa wakati wowote ambao mtumishi anaweza kupata shida kama ilivyokua hapo awali,” alisema Hilda. 

Bi. Hilda alieleza sababu ya vyama vingi vya akiba na mikopo kufa ni kitokana na uongozi mbovu, kukosekana kwa sera na mikataba isiyozingatia sheria ambayo mala zibgia inatoa miaya ya viongozi wasiokuwa waadirifu kutumika vibaya.

Hivyo aliwataka wanachama wafahamu kuwa wao ndio wanalojukumu la kuusimamia na kuulinda ushirika wao na sio kuiachia bodi. Huku akisema kuwa wao kama wasimamizi jukumu lao kuu ni kuhakikisha uendeshaji wa shughuli za chama unazingatia sheria , kanuni na taratibu zote ili kuwezeaha ushirika kuwa endelevu.

Hivyo wanachama wawe mstari wa mbele katika kuhakikisha ushirika huu ambao umesinzia kwa muda mrefu unaimarika na unakidhi mahitaji ya kuanzishwa kwake na sio kuwafaidisha wachache.

Mwenyekiti wa bodi Bw. Shija Shilagi Golani aliwaomba wanachama kushirikiana wa kutosha na mkusanya madeni aliyeletwa na Tume ya maendeleo ya ushirika kwa kipindi hiki ili aweze kutuangalizia fedga zetu.

 “Na kumuomba mwajiri atusaudie kwa wale wadaiwa ambao wanamalipo yao kwenye ofisi basi waweze kukatwa na fedha hiyo iingie kwenye akaunti ya chama,”alisema Golani.

Picha ikionesha sehemu ya wana SACCOS MWADUI wakati wa kikao cha kupokea Leseni na Cheti

 

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa