• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Waziri Biteko akataa wageni kunyenyekewa migodini

Posted on: December 11th, 2019

Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko amekataa tabia ya baadhi ya kampuni za Migodi kuwapa kipaumbele na kuwanyenyekea raia wa kigeni kuliko Watanzania.

Akizungumza na Wafanyakazi wa Mgodi wa Mwadui jana tarehe 10 Desemba, 2019 alipofanya ziara ya siku moja Mkoani Shinyanga, Mhe. Biteko amesema, kuna tabia katika baadhi ya Migodi, Watanzania wanakuwa wengi lakini maamuzi yanafanywa na watu wachache ambao mara nyingi ni raia wa kigeni hali inayosababisha wafanyakazi kukosa mahali pa kusemea changamoto zao.

Mhe. Biteko amesema Serikali ya Tanzania inataka kuona matatizo yanamalizwa bila uvunjifu wa sheria ikiwemo kuondoa manyanyaso mahali pa kazi na wafanyakazi kupata haki zao ili kuwapa motisha, kwani ndiyo wenye mchango mkubwa katika uzalishaji.

Akinukuu kifungu cha sheria ya madini ya mwaka 2017, pamoja na matakwa ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Magufuli, Mhe. Biteko amesema Watanzania wafanye kazi zozote zinaweza kufanywa na Watanzania zifanywe na Watanzania. Wageni wataajiriwa pale tu ambapo ujuzi alionao hauwezi kupatikana miongoni mwa Watanzania ikiwa ni pamoja na kuwapa mafunzo Watanzania.

"Mgeni kuwa na mshahara mkubwa ni sawa kwa sababu ametoka mbali lakini si kweli kwamba awe na mshahara mkubwa mara tano zaidi ya wenyeji, hapana tunaanza utaratibu wa kuangalia 'payrol' za wafanyakazi wa migodini" amesema Biteko.

Amesisitiza kuwa kazi yake kubwa aliyopewa ni kuhakikisha kuwa Watanzania wanafurahia maisha kwenye migodi bila kunyanyaswa na kuonewa na wageni wakipungua zaidi.

Hata hivyo, Biteko ameupongeza mgodi wa Almasi Mwadui kwa kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi pamoja na uzalishaji mkubwa wa Almasi uliofikia karati laki 4 mwaka huu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa