• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Waziri Jafo aridhishwa na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Shinyanga

Posted on: December 7th, 2019

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameipongeza Serikali ya Mkoa wa Shinyanga kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga inayojengwa katika Tarafa ya Nindo, kata ya Iselamagazi, Mkoani hapa. 

Mhe. Jafo ametoa pongezi hizo mapema leo tarehe 07/12/2019 na kusema kuwa, amefurahishwa hasa na hatua ya ujenzi ilipofikia pamoja na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua uliowekwa.

"Nakupongeza sana Mhe. Mkuu wa Mkoa na timu yako yote kwa usimamizi mzuri lakini niwapongeze na wananchi kwa kutoa eneo na kukubali Hospitali hii ijengwe hapa. Mazingira yanafurahisha kwa sababu hapakuwa hivi kabla, nimeridhika na muonekano tangu nilipokuwa nakuja" amesema Mhe. Jafo.

Jafo amesema kuwa, pamoja na shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa hapo awali kwa ajili ya kukamilisha majengo 8, Serikali itaongeza tena sh. milioni 500 hivi karibuni ili kuongeza majengo mengine.

"Tuliamua kwamba, fedha hii isije tulisubiri majengo ya kwanza yakamilike ili inapokuja awamu ya pili ifanye kazi ya kuongeza majengo mengine" amesisitiza Mhe. Jafo na kuzitaka Halmashauri nyingine waige mfano wa Halmashauri hiyo. 

Awali akitoa taarifa ya ujenzi kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Bw. Bashir Salum amesema majengo nane yamekamilika kwa shilingi Bil. 1.5 ambayo ni jengo la Utawala, Wodi ya akina mama, Maabara, Chumba cha Dawa, Chumba cha chanjo, Jengo la kufulia, Jengo la X - Ray na Jengo la kutunzia maiti.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemshukuru Mhe. Jafo kwa kutembelea Mkoa na kumuomba afanye ziara tena ili aone baadhi ya miradi ambayo imekamilika kwa kutumia mafundi wenyeji ikiwemo vituo vya Afya na Ofisi za Tarafa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa