• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WIZARA YA UJENZI NA TANROADS IMARISHENI USIMAMIZI KWA CHICO ILI UWANJA WA NDEGE UKAMILIKE HARAKA - MHE. AUGUSTINO.

Posted on: March 20th, 2025

Na. Paul Kasembo, Shy RS.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Augustino Vuma (MB) imeiagiza Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) mkoani Shinyanga kumsimamia Mkandarasi China Henan International Cooperation Group Co. Ltd (CHICO) anayetekeleza upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilishwa kwa wakati na kwa ubora uliokusudiwa ili kuleta tija ya miradi inayotekelezwa na Serikali.

Maagizo hayo yametolewa Machi 20, 2025 na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Augustino Vuma baada ya kutembelea na kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga mradi unaogharimu takribani Tzs. Bilioni 48 na ambao mpaka sasa umefikia asilimia 75% ya utekelezaji wake.

“Kamati inaiagiza Wizara ya Ujenzi na TANROADS mkoa wa Shinyanga kumsimamia Mkandarasi (CHICO) kwa ukaribu ili kuhakikisha kazi zote zilizobakia kwenye mradi huu zinakamilika kwa wakati na kwa kuzingatia ubora ili kuleta tija kwenye miradi ambayo inatekelezwa na Serikali na hatimaye wananchi ambao ndio wanufaika wakubwa wafurahie matunda yake”, amesema Mhe. Augustino.

Aidha Kamati imeiagiza Wizara ya Ujenzi, TANROADS Mkoa wa Shinyanga pamoja na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kushirikiana kwa pamoja ili kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa alipotembelea uwanja huu wa ndege na kuagiza uanze kutumika wakati wakisubiri jengo la abiria likamilike.

Aidha, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Dkt. Charles Msonde, amekiri kupokea maelekezo na ushauri wa Kamati na kuahidi kuwa watafuata maelekezo yote ikiwa ni pamoja na kumsimamia mkandarasi ili kuhakikisha utekelezaji wa mradi huu unakuwa wenye tija na unakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa.

Akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Julius Mtatiro (Wakili) ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga ameishukuru kamati kwa kutoa maelekezo haya kwani huu uwanja utakapoanza kutumika utakuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi mkoani Shinyanga.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa