• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Maktaba ya Video

  • RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA

    October 1st, 2025

    Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara za ndani katika Manispaa ya Kahama na kuagiza hatua kali zichukuliwe dhidi ya mkandarasi anayetekeleza mradi huo, Kampuni ya Sichuan Road and Bridge Group (SRBG).

    Akiwa kwenye ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo unaotekelezwa kupitia Mradi wa TACTIC iliyofanyika Septemba 30,2025 RC Mhita amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama Masoud Kibetu kuandika barua rasmi kwa mkandarasi huyo, ikiambatana na adhabu ya kukatwa milioni 2 kwa kila siku kuanzia Oktoba 1, 2025, baada ya mkataba wake kufikia ukomo tarehe 30 Septemba 2025, bila kazi kukamilika.

    “Mkandarasi huyu amelipwa zaidi ya shilingi bilioni 5, lakini kasi ya utekelezaji ni ya kusuasua licha ya kuongezewa muda mara mbili. Serikali haina tena sababu ya kumuongezea mkataba,” alisema Mhita kwa msisitizo.

    Amesema Serikali ya Mkoa haitavumilia kuona fedha za umma zinatumika bila matokeo halisi, akisisitiza kuwa kila mkandarasi anapaswa kuzingatia muda wa utekelezaji na thamani ya fedha inayotolewa kwa miradi ya maendeleo.

    Katika maagizo yake, Mhita amesisitiza kuwa adhabu hiyo ya kisheria inalenga kulinda maslahi ya wananchi ambao wanasubiri huduma bora za miundombinu na kuonya kuwa hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa endapo mkandarasi atashindwa kumaliza kazi hiyo kwa haraka.

    Ziara hiyo imekuwa sehemu ya msukumo wa kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo unakwenda kwa kasi inayostahili, huku RC Mhita akisisitiza uwajibikaji kwa watendaji wote na wadau wa ujenzi katika Mkoa wa Shinyanga

     Nao baadhi ya wananchi waliokuwepo kwenye mradi huo walimpongeza RC Mhita kwa hatua alizochukua na kumuomba kumsimamia kwa ukaribu mkandarasi huyo katika kipindi ambacho Mvua zinatarajia kunyesha ili wasipate madhara yakiwemo mafuriko kutokana na kutokamilika kwa miundombinu katika manispaa ya Kahama.

  • HATUTAKUBALI KUKWAMISHWA UJENZI BARABARA YA MWAWAZA – RC MHITA.

    September 29th, 2025

    Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita , ametembelea ujenzi wa barabara ya Mwawaza inayojengwa kwa kiwango cha lami na kutoa kauli madhubuti kuhusu umuhimu wa kukamilika kwa mradi huo kwa wakati.

    Amesisitiza kuwa hatakubali kuona mtu au taasisi yoyote ikikwamisha ujenzi huo, kwani barabara hiyo ni mkombozi mkubwa kwa wananchi, hususan wagonjwa wanaosafiri kutibiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo na wakazi wanaopata shida ya kufikika kwa urahisi.

    "Barabara hii ni uhai kwa watu wanaokwenda kutibiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ( Mwawaza) ni lazima ijengwe kwa viwango na kwa wakati. 

    Hakuna nafasi ya uzembe wala ucheleweshaji utakaokubalika kwenye ujenzi wa mradi huu," amesema RC Mhita kwa msisitizo.Ujenzi huo unatajwa kuleta mapinduzi katika sekta ya afya, biashara na usafiri kwa ujumla, na Serikali imejipanga kuhakikisha unakamilika kama ilivyopangwa.

  • SHINYANGA YANG'ARA SIKU YA USAFISHAJI DUNIANI — RC MHITA AONGOZA USAFI SOKO LA KAMBARAGE

    September 22nd, 2025

    Katika kuadhimisha Siku ya Usafishaji Duniani Septemba 20, 2025, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita ameongoza mamia ya wananchi kushiriki zoezi la usafi katika Soko la Kambarage, Manispaa ya Shinyanga.

    Akizungumza na wananchi, Mhe. Mhita amesisitiza umuhimu wa kuzingatia usafi kama sehemu ya maisha ya kila siku na si tukio la mara moja. 

    Ameeleza kuwa soko hilo ni miongoni mwa maeneo yatakayofanyiwa maboresho kupitia mradi wa TACTIC, hivyo kuhitaji maandalizi bora ya mazingira.“Tuache kusubiri maagizo, tufanye usafi kwa kujitambua, kwa afya zetu, kwa heshima ya mji wetu,” amesema RC Mhita.

    Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa CP Salum Hamduni amepongeza mwitikio wa wananchi na kutoa wito kwa jamii kuendeleza utamaduni huo kila siku.

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • Next →

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa